YANGA VS AZAM, NI FAINALI YA REKODI, KISASI


RASMI Sasa Miamba Miwili Ya Soka Nchini Yanga Na Azam Fc Zitakutana Katika Fainali Ya Kombe La Crdb (Cbfc), Ambayo Inatarajiwa Kuchezwa Juni 2, Mwaka Huu Kwenye Uwanja Wa Tanzanite, Uliopo Mjini Babati Mkoani Manyara.

Azam Ilifuzu Hatua Hiyo Baada Ya Ushindi Mnono Wa Mabao 3-0, Dhidi Ya Coastal Union Yaliyofungwa Na Nyota Wa Kikosi Hicho, Abdul Suleiman 'Sopu' Aliyefunga Mawili Na Feisal Salum 'Fei Toto', Mechi Ikipigwa Uwanja Wa Ccm Kirumba Mwanza.

Huku Yanga Yenyewe Ikifika Hapa Baada Ya Kuibuka Na Ushindi Wa Bao 1-0 Dhidi Ya Ihefu Kwenye Mchezo Mkali Uliopigwa Kwa Dakika 120 Kwenye Uwanja Wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha.

Hii Ni Fainali Ya Nne Kwa Azam Fc Katika Mashindano Haya Ambapo Mara Tatu Ilizotinga Imelichukua Mara Moja Tu Ikifanya Hivyo Msimu Wa 2018-2019, Ilipoifunga Lipuli Ya Mkoani Iringa Bao 1-0, Mechi Iliyopigwa Kwenye Uwanja Wa Ilulu Lindi.

Mchezo Huo Uliopigwa Juni Mosi, 2019, Bao Pekee La Azam Lilifungwa Na Aliyekuwa Mshambuliaji Wa Timu Hiyo Mzambia, Obrey Chirwa Dakika Ya 64.

Previous Post Next Post