BAD NEWS: AKAMATWA KWA KOSA LA KUMKATA KICHWA, VIGANJA, NYETI MTOTO WAKE


JESHI LA POLISI Mkoa Wa Morogoro Linamshikilia, Erick Julias (39) Mkazi Wa Mlimba Wilayani Kilombero Kwa Tuhuma Za Kumuua Na Kumtenganisha Kichwa Pamoja Na Viungo Vingine Mtoto Wake Wa Kufikia, Johnson Ngonyani (6).

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Leo Juni 4, 2024, Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Morogoro, Alex Mkama Amesema Pamoja Na Mtuhumiwa Huyo Kumkata Kichwa, Pia Alimkata Seheme Za Siri (Uume Na Korodani) Na Viganja Vyote Viwili.

Kamanda Mkama Amesema Mtuhumiwa Alitenda Ukatili Huo Juni 1 Mwaka Huu Majira Ya Usiku Katika Kitongoji Cha Kigamboni, Kijiji Cha Mwembeni, Mlimba Wilaya Ya Kilombero.

Amesema Mtuhumiwa Huyo Amekamatwa Kutokana Na Taarifa Za Raia Wema Na Baada Ya Kuhojiwa Polisi Amekiri Kufanya Mauaji Hayo Na Ametoa Ushirikiano Kwa Kuonyesha Sehemu Alikoficha Viungo Hivyo.

Previous Post Next Post