RUTO: "SINA HATIA" NA VIFO VYA WAANDAMANAJI

 


RAIS WA KENYA William Ruto Sasa Anadai Kuwa Hana Damu Mikononi Mwake Kufuatia Mauaji Ya Watu Yaliyoshuhudiwa Wakati Wa Maandamano Ya Hivi Majuzi.

 

Kulingana Na Ruto Ambaye Alikuwa Akizungumza Wakati Wa Kikao Na Wanahabari Katika Ikulu Jumapili, Juni 30, Maafisa Wa Polisi Walitekeleza Majukumu Yao Kwa Njia Huru Wakati Wa Maandamano Hayo.

 

Tume Ya Haki Za Kibinadamu Ya Kenya (KHRC) Katika Rekodi, Imesema Watu 23 Walifariki Kwa Kupigwa Risasi Na Polisi Kote Nchini. Zaidi Ya Hayo, Kulikuwa Na Zaidi Ya Watu 50 Waliokamatwa, 22 Kutekwa Nyara, Na Zaidi Ya 300 Kujeruhiwa.Rais Ruto Hata Hivyo Alishikilia Kuwa Ni Watu 19 Ndio Waliofariki.

 

Kuhusu Hashtag Inayovuma Ya 'Ruto Lazima Aende', Rais Alisema Kila Mtu Ana Haki Ya Kutoa Maoni Yake.

Rais William Ruto Ameeleza Nia Yake Ya Kujihusisha Na Vijana Kwenye X Space.

 

Hii Inafuatia Wito Wa Wakenya, Hasa Gen Z, Kwenye Mitandao Mbalimbali Ya Kijamii, Ambao Wamesema Kwamba Ikiwa Mazungumzo Yoyote Yatafanyika Na Serikali, Yafanywe Kwenye X Space.

 

Katika Mahojiano Na Wanahabari Jumapili, Rais Alisema Yuko Tayari Kujadili Masuala Yoyote Ambayo Wanaweza Kuwa Nayo.

 

“Nasikia Vijana Wanasema Hatutaki Jukwaa La Sektambalimbali Labda Tufanye Mazungumzo Na Rais Kwenye X. Mimi Niko Tayari Kufanya Mazungumzo Na Vijana Kwenye Jukwaa Hilo. Wakitaka Nishirikiane Nao Kwenye X, Nitakuwepo," Alisema.

 

"Nataka Tujadili Kuhusu Kodi, Nataka Tujadili Ukosefu Wa Ajira, Rushwa Na Masuala Yote."

 

Vijana Wamekuwa Wakiandaa Maandamano Nchini Kote Kwa Wiki Mbili Kuhusu Mswada Wa Fedha Wa 2024, Ambao Ruto Alioundoa Kujibu Shinikizo Zinazoongezeka.

JISAJIRI SASA NA PLAY MASTER BET - BETI KIRAHISI

BONYEZA HAPA KUJISAJIRI



Previous Post Next Post

ADVERT

ADVERT