HIVI PUNDE: MELI YA MV. CLARIAS YAZAMA

MELI YA MV. CLARIAS Iliyokuwa Kwenye Maegesho Ya Bandari Ya Mwanza Kaskazini Imekutwa Imepinduka Na Kuzama Majini Katika Ziwa Victoria Asubuhi Ya Leo Mei 19, 2024, Huku Chanzo Cha Kuzama Kwa Meli Hiyo Kikiwa Bado Hakijafahamika.

Meli Hiyo Ambayo Hivi Karibu Ilikuwa Kwenye Matengenezo Bandari Ya Mwanza Kusini, Ilihamishiwa Bandarini Hapo Tayari Kwa Kuanza Kutoa Huduma Za Usafiri Kwa Abiria Kati Ya Mwanza Na Kisiwa Cha Ukerewe.

Hata Hivyo Inaelezwa Kuwa Meli Hiyo Inaelezwa Haikua Na Abiria Yeyote Ndani.

Taarifa Zaidi Za Kuzama Kwa Meli Hiyo Zitakujia Kadri Zitakavyopatikana.

Previous Post Next Post