WAZIRI Wa Mambo Ya Nje Na
Ushirikiano Wa Afrika Mashariki, January Makamba, Amesema Tanzania Haitachoka
Kupeleka Askari Wake Kulinda Amani Katika Nchi Za Jumuiya Ya Maendeleo Kusini Mwa
Afrika (Sadc) Kwa Sababu Inaamini Katika Uhusiano Wa Kindugu, Uliowekwa Na
Waasisi Wa Taasisi Hiyo.
Akizungumza Na Mabalozi
Wa Nchi Za Sadc Wanaowakilisha Nchi Zao Jijini Beijing, China Jana, Makamba Alisema
Msingi Huo Wa Kifalsafa Ndiyo Uliofanya Tanzania Sasa Iwe Na Askari Katika Nchi
Za Jamhuri Ya Kidemokrasia Ya Congo (DRC) Na Msumbiji Baada Ya Kuombwa Kufanya
Hivyo Na Nchi Wenyeji.
“Nimekuja Hapa Kuzungumza
Nanyi Na Kuwahakikishia Kwamba Msimamo Wa Tanzania Kuhusu Sadc Haujawahi
Kuyumba Na Hautabadilika. Tatizo Lolote Litakaloikumba Nchi Ya Sadc Litachukuliwa
Kuwa Pia Ni Tatizo La Tanzania Wakati Wote,” Alisema.
Makamba Ambaye Yuko
Katika Ziara Ya Kikazi Nchini China Kufuatia Mwaliko Aliopewa Na Mwenyeji Wake
Ambaye Ni Waziri Wa Mambo Ya Nje Wa China, Wang Yi, Alisema Sadc Ni Jumuiya
Imara Kulinganisha Na Nyingine Kwa Sababu Msingi Wake Ulijengwa Katika Falsafa
Na Misingi Imara.
Akizungumza Kwa Niaba Ya
Mabalozi Wa Nchi 14 Za Sadc Waliohudhuria Mkutano Huo, Balozi Wa Namibia Nchini
China, Elia Kaiyamo, Alisema Wamefurahi Kusikia Maneno Ya Makamba Kwa Vile
Yameakisi Maneno Yaliyowahi Kutamkwa Zamani Na Baba Wa Taifa, Mwalimu Julius
Nyerere Kuhusu Umuhimu Wa Nchi Za Sadc Kuwa Pamoja.
Baadhi Ya Nchi Za Sadc Ambazo
Vikosi Vya Tanzania Vimekwenda Kuimarisha Ulinzi Ni Pamoja Na Msumbiji Na DRC Ambako
Hadi Sasa Kuna Vikosi Vya Askari Wa Tanzania Wanaoimarisha Ulinzi Na Usalama.