AJALI YAUA 13, KUJERUHI 18 MBEYA


MBEYA. “Nilisikia Kitu Kizito Kikiniangukia.” Ni Kauli Ya Mmoja Wa Majeruhi, James Mwasa Mkazi Wa Nzovwe, Jijini Mbeya Akisumulia Jinsi Ajali Hiyo Ilivyotokea Na Kusababisha Vifo Vya Watu 13 Papo Hapo Na Wengine 18 Kujeruhiwa Ikihusisha Magari Matatu, Bajaji, Pikipiki Na Guta Jijini Mbeya.

 Ajali Hiyo Imetokea Leo Jumatano Juni 5, 2024 Katika Mteremko Wa Simike, Eneo La Mbembela Likihusisha Lori Linalodaiwa Kufeli Breki Na Kwenda Kuyagonga Magari Mengine Mawili Kabla Ya Kuifikia Pikipili, Bajaji Na Guta.

Majeruhi Wa Ajali Hiyo Wamelazwa Katika Hospitali Ya Kanda, Mbeya Kwa Matibabu Zaidi, Huku Wanane Wakiwa Wamewekwa Kwenye Chumba Cha Uangalizi Maalumu (ICU).

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mbeya, Benjamini Kuzaga Ameiambia Mwananchi Kuwa Chanzo Cha Ajali Hiyo Ni Dereva Wa Lori Ambaye Alishindwa Kulimudu Baada Ya Kufeli Breki.

Amesema Dereva Wa Gari Hilo Anashikiliwa Na Polisi Kutokana Na Ajali Hiyo.

“Gari Hilo Aina Ya Scania Lilikuwa Likitokea Mbeya Kuelekea Tunduma Lilikosa Uelekeo Kutokana Na Kufeli Breki Na Likaligonga Gari Dogo Aina Ya Toyota Harrier, Kisha Kuigonga Coaster Ya Abiria Iliyokuwa Ikitokea Tunduma Kuelekea Mbeya Mjini Na Kusababisha Vifo 13 Na Majeruhi 18,” Amesema Kamanda Huyo.

Amesema Mpaka Sasa Bado Hawajajua Wapi Walipo Madereva Wa Pikipiki, Bajaj Na Guta, Kama Ni Miongoni Mwa Majeruhi Au Waliofariki Dunia.

Amesema Baadhi Ya Majeruhi Hali Zao Si Nzuri Na Jeshi La Polisi Litaendelea Kutoa Taarifa Zaidi Kadiri Zitakvyowafikia Kuhusiana Na Hali Za Majeruhi Hao.

Akizungumzia Eneo Ilipotokea Ajali, Kamanda Kuzaga Amesema Ni Korofi Na Mara Zote Askari Wa Usalama Barabarani Hutoa Tahadhari Kwa Madereva Kuwa Makini Wanapolifikia Eneo Hilo Pamoja Na La Mlima Shamwengo.

“Zipo Hatua Tunachukua Kwa Madereva, Ikiwamo Kuwapatia Elimu, Lakini Hapa Ni Eneo Lenye Mteremko Mkali Na Kuna Ujenzi Wa Barabara Wa  Njia Nne Unaendelea, Ukikamilika Huenda Ajali Kama Hizi Zinazokatisha Uhai Wa Watu Wengi Kwa Wakati Mmoja Zitapungua Kwa Kiwango Kikubwa,” Amesema Kamanda Huyo.

Previous Post Next Post