ELON MUSK HAKUALIKWA KWENYE MKUTANO MKUU WA UWEKEZAJI WA UINGEREZA

TAJIRI zaidi duniani, Elon Musk, hajaalikwa kwenye Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji wa serikali ya Uingereza ikiwa ni hatua ya kujibu ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii wakati wa ghasia za mwezi uliopita.

Ghasia zilienea kote Uingereza baada ya shambulio la kisu huko Southport, ambapo watoto watatu waliokuwa wakihudhuria darasa la kucheza densi waliuawa.

Mjasiriamali huyo wa teknolojia aliweka kwenye mtandao wa X, ambao zamani ulijulikana kama Twitter, ujumbe akitabiri vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Uingereza na kumshambulia mara kwa mara waziri mkuu.

Mkutano wa kilele mwezi Oktoba ni wakati muhimu ambapo Waziri Mkuu Keir Starmer anatumai kuvutia makumi ya mabilioni ya fedha kwa ajili ya biashara kutoka kwa wawekezaji wakubwa duniani.

Bw Musk alihudhuria hafla ya mwaka jana na kuchukua jukumu muhimu katika mkutano wa akili mnemba - AI wa Novemba, ikiwa ni pamoja na mazungumzo ya kusisimua ya pembeni na Waziri Mkuu wa wakati huo Rishi Sunak.

Serikali na Bw Musk wametafutwa ili kutoa maoni yao.

Wakati wa ghasia za Agosti, Bw Musk alishirikisha, na baadaye kufuta maoni yake kuhusu fikra za njama ya Uingereza kujenga "kambi za kizuizini" katika Visiwa vya Falkland kwa ajili ya waasi, kwenye mtandao wa X - jukwaa analomiliki.

Wakati huo mawaziri walisema maoni yake "hayana msingi wowote" na ni "ya kusikitisha sana."

Huenda hii ndiyo sababu hajaalikwa kuungana na mamia ya wawekezaji wakubwa duniani katika hafla hiyo ya tarehe 14 Oktoba.

JISAJIRI SASA NA PLAY MASTER BET - BETI KIRAHISI

BONYEZA HAPA KUJISAJIRI



Previous Post Next Post

ADVERT

ADVERT